Katibu mkuu wa jumuiya ya nchi zinazozalisha mafuta OPEC Bw. Mohammed Barkindo amesema, akiba ya mafuta itaendelea kupungua, na kupandisha bei ya mafuta katika nusu ya pili ya mwaka huu.
Kwenye mkutano wa 22 wa mafuta duniani uliofanyika huko Istanbul, Bw. Barkindo amesema pande mbalimbali zitatekeleza makubaliano yaliyofikiwa mwaka jana na nchi za OPEC na nchi zinazozalisha mafuta zisizo wanachama wa OPEC kuhusu kupunguza uzalishaji wa mafuta, ili kuongeza bei ya mafuta.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |