Tanzania: Kampuni ya Simu ya China, Huawei imeingia makubaliano na kampuni ya huduma ya kutuma fedha kwa simu ya WorldRemit kuwawezesha wateja kutoa na kupokea fedha nje ya Bara la Afrika.
Huduma hiyo itawawezesha wateja waliopo barani Afrika kupokea fedha moja kwa moja kwa njia ya simu kutoka nchi zilizopo nje ya Afrika kwa urahisi zaidi tofauti na ilivyo sasa.
Makamu wa Rais wa Huawei, David Chen amesema hatua hiyo itasaidia kuziunganisha akaunti zaidi ya 100 milioni kupitia kampuni hiyo na kurahisisha huduma za kifedha.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |