• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Kesi zaidi ya elfu 13 kuhusu rasilimali za maingira zilisikilizwa mwaka jana

    (GMT+08:00) 2017-07-13 19:09:59
    Kesi zaidi ya elfu 13 zinazohusiana na rasilimali za mazingira zilisikilizwa kuanzia mwezi Julai mwaka jana mpaka mwezi Juni mwaka huu nchini China.

    Waraka maalum uliotolewa na Mahakama Kuu ya China umesema, watu zaidi ya elfu 27 wamehukumiwa, huku idadi ya kesi za uhalifu wa aina hiyo zilizofunguliwa zimefikia 16,373. Waraka huo pia umesema mahakama katika ngazi zote zimeimarisha kusikiliza kesi za raia zinazohusiana na masuala ya mazingira.

    Pia, kituo cha utafiti wa sheria kuhusu rasilimali za mazingira katika Mahakama hiyo, leo kimetoa mwendelezo wa ripoti kuhusu sheria ya mazingira nchini China, na kutoa wito wa sheria kuhusu uwajibikaji na kuboresha mfumo huo kwa ajili ya usimamizi wa kufungua kesi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako