Ikulu ya Ufaransa imetangaza kuwa nchi hiyo na Ujerumani zitashirikiana kwenye kusanifu na kutengeneza ndege za kivita za kizazi kipya za Ulaya, na pande hizo mbili zinatarajia kukamilisha mpango wa kutekeleza mradi huo mwakani. Rais Emanuel Macron wa Ufaransa amesema mradi huo ni jukumu kubwa na gumu kwa Ufaransa na Ujerumani, na ndege mpya zitatumiwa na majeshi ya nchi hizo mbili. Chansela wa Ujerumani Bibi Angela Merkel amesisitiza kuwa nchi hizo mbili zitaendelea kushiriki kwenye utafiti wa ndege zisizo na rubani za kivita za Ulaya, na kuimarisha ushirikiano kati yao katika teknolojia ya satelaiti na dijitali, na usalama wa mtandao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |