Mshambuliaji wa zamani wa Klabu ya Manchester United Wayne Rooney na kiungo Kieran Dowell walipachika bao moja kila moja na kusaidia Everton kuzima Gor Mahia 2-1.
Timu zote zilianza vizuri kabla ya Gor kuimarika. Hata hivyo, Everton ilizidi nguvu Gor, ambayo ilijikatia tiketi ya kumenyana na klabu hiyo ya Uingereza baada ya kuaibisha mahasimu wa jadi AFC Leopards 3-0 katika fainali ya shindano la SportPesa Super Cup nchini Tanzania hapo Juni 11.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |