Polisi nchini Israel jana walifungua msikiti wa Al-Aqsa na kuimarisha hatua za ulinzi kwenye eneo hilo, licha ya hatua hizo kususiwa na mamlaka ya usimamizi wa taasisi za kidini, na kiongozi wa msikiti huo amewataka waumini wasiende kwenye msikiti huo hadi polisi wa Israel watakapoondoa zana na kamera mpya za kiusalama zilizowekwa langoni mwa msikiti huo. Polisi nchini Israel waliamua kufunga msikiti wa Al-Aqsa baada ya polisi watatu kuuawa kwa kupigwa risasi kwenye eneo hilo Ijumaa iliyopita.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |