• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Waziri wa fedha wa Uingereza asema Uingereza inapaswa kufikia makubaliano ya mpito na EU

    (GMT+08:00) 2017-07-17 09:49:58

    Waziri wa fedha wa Uingereza Bw Philip Hammond, amesema Uingereza inapaswa kufikia makubaliano ya mpito na Umoja wa Ulaya, ili kuyapatia makampuni muda wa mpito ili isije ikatokea hali ya kuondoka ghafla kutoka Umoja wa Ulaya.

    Bw. Hammond alipohojiwa na shirika la utangazaji la Uingereza BBC amesema wiki kadhaa zilizopita kulikuwa na wazo jipya la kuweka muda wa mpito kwa Brexit, lakini kwa sasa watu wengi wanakubalia wazo hilo. Kuweka muda wa mpito kutaifanya Uingereza itumie mpango wa sasa ipasavyo, ili kupunguza athari kwa uendeshaji wa makampuni.

    Waziri wa Brexit wa Uingereza David Davies atakwenda Brussels leo, kufanya mazungumzo ya duru ya pili na Umoja wa Ulaya.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako