• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rais wa Uturuki kupendekeza kurefusha hali ya dharura

    (GMT+08:00) 2017-07-17 10:10:59

    Mkutano wa mwaka mmoja tangu kushindwa kwa mapinduzi ya kijeshi ya Uturuki umefanyika mbele ya bunge la Uturuki huko Ankara. Rais Recep Tayyip Erdoğan amehudhuria mkutano huo na kupendekeza kurefusha hali ya dharura.

    Rais Erdogan ametoa hotuba katika mkutano huo akisisitiza kuwa moyo thabiti wa kuunga mkono umoja wa mamlaka na demokrasia wa wananchi wa Uturuki. Amesema maadui hawawezi tena kuigawa nchi hiyo, na hataruhusu mapinduzi ya kijeshi kutokea tena.

    Pia amesema kamati ya usalama ya taifa itaitisha mkutano kupendekeza kurefusha hali ya dharura kwa miezi mingine mitatu, na pendekezo hilo litawasilishwa kwenye baraza la mawaziri na halafu kujadiliwa bungeni.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako