• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rwanda: Wanawake wafanya biashara wa Rwanda walalamikia mazingira duni

    (GMT+08:00) 2017-07-19 19:07:47

    Wanawake wafanya biashara wa Rwanda wanaovuka mipaka kufanya shughuli zao kwenye kanda ya Afrika Mashariki wameomba serikali za kanda hiyo kuweka mazingira mazuri kwao.

    Wanawake hao ambao wengi wanavuka mipaka maeneo ya Rusizi-Bukavu na Rubavu-Goma wanalalamikia kuongezeka kwa ufisadi, dhuluma za kingono na ukosefu wa mtaji wa kutosha wa kufanya biashara.

    Mwenyekiti wa chama cha wanaouza nyanya na kitunguu Janet Mukamunana amesema matukio hayo yameathiri vibaya biashara zao.

    Amesema pia imekuwa vigumu kushindana na wenzao wa DR Congo ambao pia wana bidhaa sawa na zao.

    Wengi wa wanawake wanafuka mipaka kufanya biashara ndogondogo kama vile kuuza samaki, maziwa, nyanya na matunda.

    Sasa wizara ya biashara viwanda na maswala ya Afrika Mashariki pamoja na wizara ya maswala ya kijinsia zimemesa zinajitahidi kuboresha mazingira ya biashara kwa wanawake hao .

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako