Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika SADC imekataa ombi la Burundi la kujiunga na jumuiya hiyo kwa kudai kuwa nchi hiyo bado haijakidhi vigezo vinavyotakiwa. Mwenyekiti wa kamati ya mawaziri wa SADC inayoshughulikia siasa na ushirikiano wa ulinzi na usalama Dk. Augustine Mahiga amesema hali ya kisiasa nchini Burundi bado haijatulia kuiruhusu nchi hiyo ijiunge na jumuiya hiyo ya kikanda. Burundi imeshuhudia msukosuko wa kisiasa tangu vurugu ziibuke miaka miwili iliyopita baada ya rais Pierre Nkurunziza kunyakua urais kwa muhula wa tatu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |