Kushinda medali yake ya kwanza ya dhahabu ilikuwa ndoto kubwa kutimia kwa bingwa wa riadha za walemavu duniani David Emong wa Uganda lakini anasema bado hajatosheka
Akizungumza baada ya kuwasili nyumbani Uganda kutoka London alikoshiriki mashindano ya walemavu, Emong alisema bado anapania kushinda medali ya dhahabu zaidi katika matukio ya baadaye ya mashindano ya kimataifa.
Alisema ushindi wake ni mwanzo tu kwani anataka kushinda medali za dhahabu katika mashindano ya Jumuiya ya Madola itakayofanyika Tokyo mwaka 2020 na matukio mengine ya kimataifa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |