Watu zaidi ya 11 wamefariki na wengine 29 wamejeruhiwa katika ajali ya lori, katika eneo la Mazabuka, Zambia.
Kamishna wa polisi Bw Bonnie Kapeso amesema, lori moja lililobeba watu 40 lilianguka kwenye mfereji wa maji wakati wa usiku na kusababisha vifo vya wanaume 6, wanawake wawili na watoto watatu.
Habari kutoka polisi zimesema, ajali hiyo imetokana na dereva kutokuwa mzoefu.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |