Wahamiaji tisa wanaume wamethibitishwa kufariki dunia baada ya kukwama ndani ya tela la trakta kwenye eneo la maegesho la supamaketi ya Walmart mjini San Antonio, Taxas. Kwa mujibu wa wizara ya usalama wa ndani, watu wengine wapatao 30 waliogunduliwa wakiwa hai kwenye tela hiyo wamekimbizwa hospitali. Mpaka sasa polisi bado hawajathibitisha wahamiaji hao wanatoka nchi gani na wanaelekea wapi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |