Shambulizi la ufyatuaji risasi lilitokea jana ndani ya ubalozi wa Israel mjini Amman, Jordan na kusababisha kifo cha raia mmoja wa Jordan na wengine wawili kujeruhiwa.
Idara ya usalama wa umma ya Jordan imesema shambulizi hilo limetokea katika jengo la makazi lililoko ubalozi wa Israel, na majeruhi wamekimbizwa hospitali.
Hivi sasa polisi wamezingira maeneo yaliyoko karibu na ubalozi huo na uchunguzi bado unaendelea.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |