• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • IMF yasema uchumi wa dunia bado unaendelea kukua

    (GMT+08:00) 2017-07-24 19:32:15
    Shirika la Mfuko wa Fedha la Kimataifa leo limetoa ripoti ikisema ukuaji wa uchumi duniani bado unaendelea kupanda, na kukadiria kuwa utadumisha kiwango chake cha asilimia 3.5 na 3.6 kwa mwaka 2017 na 2018.

    Ripoti imesema Kutobadilika kwa makadirio hayo kunatokana na sababu tofauti kwa mujibu wa nchi, ambapo kimsingi inaonesha ni matokeo ya kubadili sera za uchumi katika nchi mbili zenye uchumi mkubwa, Marekani na China.

    Ripoti imekadiria kuwa ukuaji wa uchumi wa China kwa mwaka 2017 utapanda kwa asilimia 0.1 na kufikia asilimia 6.7 kutoka Aprili, ikionesha uimara katika robo ya kwanza. Kwa upande wa Marekani makadirio yanaonesha kushuka kutoka asilimia 2.3 ahadi 2.1 mwaka huu, na kutoka asilimia 2.5 hadi 2.1 mwaka 2018. Ripoti imesema nchi nyingine yenye ukuaji mdogo ni Uingereza ukiwa na ukuaji dhaifu kuliko ilivyotarajiwa katika robo ya kwanza.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako