Jumla ya waethiopia elfu 70 wamerudi nyumbani, wakati muda wa msamaha uliotolewa na serikali ya Saudi Arabia kwa wahamiaji haramu kuondoka kwa hiari umekwisha jana. Msemaji wa Wizara ya mambo ya nje ya Ethiopia Bw Meles Alem amesema hivi sasa serikali ya Ethiopia inafuatilia kazi ya kuwarudisha raia wengine elfu 60 wa nchi hiyo walioandikishwa na ubalozi wa Ethiopia nchini Saudi Arabia. Idadi ya jumla ya waethiopia wanaoishi kiharamu nchini Saudi Arabia inakadiriwa kuwa ni laki nne, ambao wanajishughulisha na kazi mbalimbali kama vile wahudumu na wajenzi.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |