Rais Recep Erdoğan wa Uturuki jana aliwasili nchini Qatar baada ya kumaliza ziara nchini Saudi Arabia na Kuwait, ikiwa ni mwendelezo wa juhudi zake za kusuluhisha mgogoro wa kidiplomasia kati ya Qatar na nchi nne za kiarabu. Kwenye ziara hiyo, rais Erdogan amekutana na kiongozi mkuu wa Qatar Tamim bin Hamad Al Thani, na kubadilishana naye maoni kuhusu jinsi ya kutatua mgogoro huo. Qatar ni kituo cha mwisho cha ziara ya rais Erdogan katika nchi tatu za ghuba.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |