Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Iran amesema balozi wa Iran nchini Kuwait ataendelea na majukumu yake nchini Kuwait, na ujumbe wa kidplomasia wa Iran nchini humo utaendelea kuwa wa ngazi ya kibalozi. Msemaji huyo amesema ingawa idadi ya wanadiplomasia wa Iran nchini Kuwait imepungua, lakini hakuna wanadiplomasia wa Iran waliofukuzwa au kuorodheshwa kuwa ni "watu wasiokaribishwa", na kwamba nchi hizo mbili zitaendelea na mawasiliano na mazungumzo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |