FUFA ilitarajiwa kutoa mwelekeo kuhusu hatma ya kocha huyo hapo jana lakini ikatoa taarifa tu kusema mazungumzo baina yake na Micho bado yanaendelea, huku wakala wa kocha huyo akidokeza kuwa uamuzi huo utafanywa karibuni.
Wikendi iliyopita, Micho alitangaza nia yake ya kutoendelea kuifunza timu ya Cranes kutokana na kutokuelewana baina yake na usimamizi wa soka nchini humo akidai kuwa malimbikizo yake hayajashughulikiwa ipasavyo na shirikisho la soka nchini Uganda FUFA.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |