• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Wakulima Tanzania kunufaika na mbegu zinazovumilia ukame

    (GMT+08:00) 2017-07-25 19:17:32

    Wakulima wanatarajia kunufaika na kazi za mikono yao baada ya kupatikana kwa mbegu zinazovumilia ukame na magonjwa, jambo litakaloongeza mavuno.

    Kuongezeka kwa mavuno kutapandisha kipato cha wakulima hao, hivyo kuwapa nafasi ya kutumia fursa za kujenga viwanda vidogo vitakavyoongeza thamani ya mazao yao na kuleta mapinduzi kwenye sekta hiyo inayotoa ajiri kwa zaidi ya asilimia 80 nchini.

    Kupitia Mpango wa Kusaidia Biashara na Kilimo (TASP) unaofadhiliwa na Jumuiya ya Ulaya, Taasisi ya Utafiti wa Chai (Trit), inasema imefanikiwa kuzalisha aina nne za miche ya chai itakayoongeza tija kwa mkulima. Pia, imefanikiwa kuwaunganisha wakulima na kujenga ghala la pembejeo Wilayani Mufindi linalohudumia zaidi ya wakulima 1,200.

    Mkurugenzi Mtendaji wa Trit, Dk Emmanuel Simbua akizungumza na Gazeti hili hivi karibuni, alisema vituo 20 vya kupimia hali ya hewa vimewekwa katika maeneo yanayozalisha chai ili kuwasaidia wakulima.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako