Ofisi ya waziri mkuu wa Israel imetoa taarifa ikisema, wafanyakazi wote wa ubalozi wa nchi hiyo nchini Jordan wamerejeshwa nyumbani jana usiku.
Taarifa hiyo imesema, wafanyakazi hao ni pamoja na balozi Bw. Einat Schlein na ofisa mmoja wa usalama aliyejeruhiwa. Kurudi nyumbani kwa usalama kwa wafanyakazi hao ndani ya saa 24 kunatokana na ushirikiano wa karibu kati ya nchi hizo mbili.
Waziri mkuu wa Israel Bw. Benjamin Netanyahu ametoa salamu za pole kwa Bw. Schlein na ofisa wa usalama aliyejeruhiwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |