• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Muundo wa ushirikiano kwa pande zote kati ya majeshi ya China na Russia waanzishwa hatua kwa hatua

    (GMT+08:00) 2017-07-26 18:19:16

    Huu ni mwaka wa 90 tangu kuanzishwa kwa jeshi la ukombozi la umma la China. Katika miaka 90 iliyopita, jeshi la China limekuwa likiimarisha ushirikiano wa kijeshi na usalama na nchi mbalimbali duniani, ambapo majeshi ya China na Russia yamejenga utaratibu wa ushirikiano katika sekta mbalimbali na wa kiwango cha juu. Katika miaka ya hivi karibuni, nchi hizo mbili zimefanya luteka nyingi za pamoja za kijeshi, na mawasiliano ya kijeshi yamekuwa yakiimarishwa. 

    Uhusiano kati ya majeshi ya China na Russia unachukua sehemu muhimu katika uhusiano wa ushirikiano wa kimkakati na kiwenzi kwa pande zote kati ya nchi hizo mbili. Katika miaka ya hivi karibuni, mawasiliano ya ngazi ya juu kati ya majeshi ya nchi hizo mbili yamekuwa yakiimarishwa siku hadi siku, kuaminiana kimkakati kumezidi kuimarika, ushirikiano katika sekta za kitaaluma unafanyika kwa ufanisi mkubwa, na uhusiano wa majeshi hayo unapata maendeleo katika maeneo mengi zaidi. na kwa kina zaidi. Mwambata wa kijeshi katika ubalozi wa China nchini Russia Bw. Wei Yanwei anasema:

    "Hivi sasa majeshi ya China na Russia yanafanya ushirikiano wenye ufanisi katika sekta mbalimbali ikiwemo mawasiliano ya ngazi ya juu, luteka na mafunzo kwa pamoja, kufanya mawasiliano ya kitaaluma, mikutano ya kimataifa, mashindano ya kijeshi ya kimataifa, ushirikiano wa teknolojia za kijeshi, pamoja na mafunzo kwa wataalamu, ambapo muundo wa pande zote umeanzishwa hatua kwa hatua."

    Bw. Wei ameeleza kuwa, mwezi Juni mwaka huu, mawaziri wa ulinzi wa China na Russia walisaini Mpango wa maendeleo ya ushirikiano

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako