• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Bunge la Uganda lamfulia kofia Emong

    (GMT+08:00) 2017-07-27 10:30:33
    Bunge la Uganda limempongeza na kumtaja mwanariadha David Emong kama shujaa anayestahili heshima kutoka kwa Waganda wote baada ya kushindia Uganda medali ya dhahabu katika mashindano ya dunia ya riadha ya walemavu yaliyofanyika Julai 15 jijini London.

    Wabunge walisema Emong aliiletea Uganda sifa baada ya kumpiku bingwa mtetezi Samir Nouioua kutoka Algeria.

    Mbunge wa kaunti ya Kioga Anthony Okello, aliwasilisha hoja bungeni kushinikiza kutambuliwa kwa Emong wakati wa kikao cha jana. Hoja hiyo iliungwa mkono na wabunge wengi ambao walitoa wito kwa serikali kujenga nyumba kwa Emong na pia kununua gari kwa ajili yake jinsi ilivyofanyika kwa wanariadha wengine kama vile bingwa wa riadha duniani mwaka 2013 Stephen Kiprotich.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako