• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • IAAF kutuza Mkenya Paul Tergat

    (GMT+08:00) 2017-07-27 10:30:53

    Shirikisho la kimataifa la riadha duniani IAAF inalenga kumtunuku bingwa mara tano wa dunia katika mashindano ya marathon Paul Tergat na tuzo la PIN kwa mchango wake bora katika riadha

    Tergat atatunukiwa tuzo hilo la kifahari Agosti 1 katika hafla ya ufunguzi wa Makala ya 51 ya Congress, inayotangulia mashindano ya riadha ya dunia yatakayofanyika jijini London.

    Tergat ambaye ni mwanzilishi wa tuzo la Sports Personality of the Year Awards (Soya), amekuwa maarufu kwa ulimwengu wa riadha kitaifa na kimataifa kwa mchango wake wa thamani ambayo sasa umefanya usimamizi wa riadha duniani kutambua mchango wake.

    Tergat ambaye ni mshindi mara 13 kwa mbio za Marathon duniani ni mwanachama wa kamati ya Olimpiki (IOC) na kwa sasa anawania wadhifa wa mwenyekiti wa kamati ya Olimpiki nchini Kenya NOCK, wadhifa ambao anatarajiwa kushinda baada kuidhinishwa bila kupingwa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako