Kampuni ya Jambo Jet itakuwa na safari 5 mpya za ndege kila wiki kuanzia mwezi huu kutokana na ongezeko la idadi ya abiria Eldoret.
Kampuni hiyo sasa itakuwa na jumla ya safari 18 kila wiki kutoka Nairobi hadi Eldoret .
Hatua hii inajiri licha ya hofu ya kampuni hii ya kupunguza huduma zake kutokana na ratiba ya uchaguzi mkuu.
Usimamizi wa kampuni hiyo umeelezea pia safari hizo zimejiri kufuatia kuimarika kwa biashara katika kaunti ya Eldoret.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |