Polisi wa Israel wamesema, vifaa vyote vipya vya kiusalama vilivyowekwa kwenye eneo la Temple Mount vimeondolewa na hatua zote za kiusalama zimerudishwa kama ilivyokuwa kabla ya kutokea kwa shambulizi Julai 14.
Wapalestina wengi walikusanyika katika eneo hilo kushuhudia na kusherehekea kuondolewa kwa vifaa hivyo.
Habari zinasema katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Bw António Guterres ametoa taarifa kupitia msemaji wake, akikaribisha kurejeshwa kwa utulivu katika eneo hilo la Jerusalem. Pia anatarajia kuwa pande zote husika zitaendelea kufanya mazungumzo ili kuongeza uaminifu kati yao.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |