Wafanyabiashara wanaojihusisha na biashara ya dhahabu nchini Ethiopia wamelalamikia hatua ya kuongezwa kwa kodi inayotozwa na serikali. Kwenye mageuzi ya utoaji kodi yaliyofanywa hivi majuzi, serikali iliongeza viwango hivyo kwa hadi mara nne ikiwa ni zaidi ya kiwango kinachotozwa kwa sasa. Kwa muda wa miezi miwili, wafanya biashara wamekuwa wakifunga maduka yao katika miji kadhaa baada ya mpango huo mpya kuanza kutekelezwa. Baadhi ya miji hiyo ipo katika eneo la Oromia ambako kuliutokea maandamano makubwa dhidi ya serikali mnamo 2015 baada ya kutangazwa kwa hali ya hatari.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |