Timu ya viliboli ya Rwanda ya chipukizi wasiozidi miaka 20 liliondoka jumapili usiku kuelekea Senegal itakaposhiriki mashindano ya mwaka huu ya IHF Continental Phase – Africa ambayo imeratibiwa kuanza Agosti 1-5 jijini Dakar.
Timu hiyo yenye wachezaji 14 inayofunzwa na kocha Antoine Ntabanganyimana, imekuwa kwenye kambi ya mazoezi tangu Julai 16 kujiandaa kwa mashindano hayo. Timu hiyo itakayoshiriki mashindano hayo kwa mara ya kwanza, ilifuzu baada ya kushinda Uganda Disemba mwaka uliopita.
Rwanda imewekwa kwenye kundi A na inaanza kampeini yake kwa kuchuana na timu kutoka Madagascar kesho Jumanne kabla ya kukutana na timu kutoka Demokrasia ya Kongo DRC siku moja baadaye kabla ya kumaliza mechi za raundi dhidi ya Senegal.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |