Dhamani ya hisa za kampuni ya mawasiliano nchini Kenya Safaricom imeongezeka sasa kwa jumla ikiwa ni dola bilioni 2 mwaka huu.
Ijumaa iliopita hisa moja ya kampuni hiyo iliuza kwa dola 0.24 sawa na shilingi 25.
Hisa za kampuni hiyo zimekuwa zikifuatiliwa sana hasa na wawekezaji wa kigeni na mwaka huu zimekuwa na ongezeko la dhamani la asilimia 28.
Safaricom aidha ndio kampuni yenye faida kubwa zaidi nchini Kenya na kwenye soko la hisa ina dhamani ya asilimia 42.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |