• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Tanzania: Mamlaka ya Anga Tanzania (TCAA) kununua rada nne

    (GMT+08:00) 2017-08-01 19:21:49

    Mamlaka ya Usafiri wa Anga Nchini Tanzania (TCAA), inatarajiwa kununua rada nne kwa ajili ya kumulika anga la Tanzania mpaka nje ya nchi.

    Kwa mujibu wa Mwanasheria Mwandamizi wa TCAA, Maria Memba, rada iliyonunuliwa hivi karibuni ni ya mwaka 2002.

    Alisema ili kukamilisha ununuaji wa rada hizo, TCAA ipo katika hatua za kukamilisha mkopo, utakaowawezesha kununua rada hizo kwa gharama za Euro milioni 22 (Sh bilioni 43).

    Mkurugenzi Mkuu wa TCAA, Hamza Johari alinukuliwa akisema mradi huo ukikamilika utakuwa na faida nyingi kiusalama, kwani kwa kutumia rada mwongoza ndege anaweza kuongoza ndege nyingi zaidi kwa ufanisi na kuongeza mapato.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako