Kulingana na taarifa kutoka TFF, kamati ya utendakazi ya shirikisho hilo lilikutana karibuni na kumteua wakili Damas Ndumbaro kama mwenyekiti wa kamati hiyo.
Ndumbaro anarejea kwenye wadhifa huo baada ya kamati ya nidhamu ya TFF kuondoa marufuku hivi majuzi iliyokuwa imemwekea. Sasa Ndumbaro atasaidiwa na wakili Alex Mgongolwa.
Kamati hiyo inajukumu la kushughulikia rufaa kutokana na maamuzi yanayofanywa na kamati ya kutoa leseni kwa vilabu. Kulingana na kanuni mpya, vilabu vyote vinavyoshiriki daraja ya juu, vinahitajika kutuma maombi ya kupewa leseni mpya kwa muda ambao umetangazwa na kamati ya utendakazi ya TFF.
Aidha vilabu hivyo vinatakikana kuhakikisha kuwa vimeitimu mahitaji yote ili kupokea leseni hiyo ya kushiriki ligi, la sivyo vitashushwa daraja.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |