• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Micho kuingia Orlando Pirates

    (GMT+08:00) 2017-08-03 10:29:54
    Aliyekuwa kocha wa timu ya soka ya taifa ya Uganda Micho Sredojevic sasa anatarajiwa kujiunga na klabu ya Orlando Pirates ya Afrika Kusini siku chache baada ya kuitimisha mkataba wake na timu ya Uganda Cranes.

    Micho aliondoka Cranes wiki hii kutokana na mzozo baina yake na shirikisho la kandanda nchini Uganda FUFA kuhusiana na marupurupu yake kwa muda ambao alihudumu kama mkufunzi wa timu hiyo.

    Micho alidai kuwa FUFA ilishindwa kumlipa hela zake na hivyo hakuwa na budi ila kuondoka. Na sasa duru zinaarifu kwamba klabu yake ya zamani ya Orlando Pirates imeweka mpango mahsusi kumpa kandarasi kocha huyo Raia wa Serbia.

    Taarifa hizi zilishika kasi hasa baada ya kocha wa klabu hiyo Kjell Jonevret kujiuzulu wadhifa huo na kuacha pengo. Micho pia anasemekana kuwa rafiki wa Karibu wa mmiliki wa klabu hiyo Irvin Khoza.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako