Mashindano ya mwaka huu ya wanaume ya bara Afrika yameratibiwa kufanyika kuanzia Septemba 6 hadi 16 nchini Senegal na Tunisia. Kampuni ya Star Times imepewa kibali kupeperusha mashindano hayo rasmi.
Rwanda ilijikatia tikiti kuingia mashindano hayo na FIBA Africa baada ya kushindwa kufuzu moja kwa moja kutoka mashindano ya Zone V Championship yaliyofanyika Misri mapema mwaka huu.
Timu hiyo sasa imepangiwa kuanza mazoezi rasmi siku ya Jumatatu kwenye uwanja wa Amahoro.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |