Awamu ya pili ya kongamano la kila mwaka la masuala ya uchumi Afrika litajadili zaidi masuala ya uwekezaji .
Kongamano hili litakalofanyika Miasri kuanzia disemmba 7 hadi 9 litafunguliwa kwa mjadala wa vijana na ujasiriamali kwani ndio sekta inayotarajiwa kutawala uchumi wa Afrika miaka ijayo.
Kongamano hilo mwaka huu litarajiwa kuvutia wajasiriamali,wataalamu,wawekezaji na wabunifu wa ajira.
Wizara ya biashara na uchumi ya misri imearifu uwepo wa jamii ya kimataifa ya uwekezaji ,shirika la kimataifa la uwekezaji pamoja na viongozi wa biashara duniani.
Waziri wa biashara na uwekezaji Sahar Nasr amesema watazingatia fursa za uwekezaji Afrika ili kulikwamua bara hili kutokana na mfumko wa uchumi.
Maudhui makuu itakuwa mbinu za kupatikana kwa mabadiliko uhimu ya mazingira ya biashara na mbinu za kuliweka bara la Afrika kwenye ramani ya upinzani wa biashara duniani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |