Shirika la Umoja wa Mataifa ya Elimu, Sayansi na Utamaduni UNESCO limeeleza wasiwasi kwamba uharibifu kwenye Reli ya Darjeeling Himalaya nchini India unatishia heshima ya urithi huo wa dunia. Vituo viwili muhimu vya reli hiyo vilichomwa moto wakati jaribio la uchomaji lilifanyika kwenye jengo la Elysia, wakati wa mgomo uliotokea kwenye jimbo la mashariki nchini humo. Afisa wa UNESCO Bw. Moe Chiba amesema kutokana na uharibifu huo, mkutano wa pili wa Kamati ya Urithi wa Dunia utakaofanyika mwaka 2018 utafanya ukaguzi tena kuhusu urithi huo.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |