Kesi ya utakatishaji pesa inayomkabili rais wa klabu ya simba Evans Aveva na makamu wake Geoffrey Nyange maarufu Kaburu, iliendelea katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ambapo imeahirishwa hadi August 16, 2017 kwa sababu upelelezi haujakamilika.
Hayo yalielezwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Godfrey Mwambapa na Wakili wa Serikali, Elia Athanas ambaye amedai Mahakamani hapo kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika hivyo anaomba ipangiwe tarehe nyingine ambapo Hakimu Mwambapa aliahirisha kesi hiyo hadi August 16, 2017.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |