• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Rais Zuma wa Afrika Kusini anusurika kwa mara ya nane kwenye kura ya kutokuwa na imani naye

    (GMT+08:00) 2017-08-09 09:45:20

    Bunge la Afrika Kusini limepiga kura ya siri kuhusu kukosa imani na rais Jacob Zuma, ikiwa ni mara ya nane kupigiwa kura hiyo. Kutokana na kura hizo kutofikia zaidi ya nusu ya wabunge, mswada huo haukupitishwa

    Spika wa bunge Bibi Baleka Mbete, amesema kati ya wabunge 384 waliopiga kura, wabunge 198 walipiga kura ya kupinga mswada huo, wengine 177 walipiga kura ya kuunga mkono mswada huo, na wabunge 9 waliacha kupiga kura.

    Baada ya upigaji kura huo, chama tawala cha ANC kimetoa taarifa kikisema, licha ya kuwa kuna masuala mengi nchini Afrika Kusini, lakini mafanikio yaliyopatikana chini ya uongozi wa chama hicho hayawezi kukanushwa.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako