Madrid walidhibiti mchezo huo kuanzia kipenga cha kwanza na kwa haraka wakajipata kifua mbele pale Casemiro alipowafungia bao, muda mfupi baada ya kugonga mwamba wa goli.
Waliongeza la pili kupitia Isco aliyefunga akiwa hatua nane kutoka kwenye goli baada ya kubadilishana pasi na Gareth Bale, ambaye alichezeshwa safu ya mashambulizi badala ya Cristiano Ronaldo.
Mshambuliaji wa United Romelu Lukaku, aliyenunuliwa milioni 75 pauni ya Uingereza, alikomboa bao moja lakini Marcus Rashford akapoteza fursa nzuri ya kufunga kwa kuutuma mpira nje.
Madrid ni timu ya kwanza kufanikiwa kutetea Kombe la Super Cup la Uefa tangu 1990. Mechi hiyo ilichezwa chini ya joto kali la nyuzi joto 30 katika mji mkuu huo wa Macedonia.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |