• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • China yaadhimisha miaka 70 tangu kuanzishwa kwa mkoa unaojiendesha wa Mongolia ya Ndani

     

    (GMT+08:00) 2017-08-09 18:19:09
    Mkutano wa kuadhimisha miaka 70 tangu mkoa unaojiendesha wa Mongolia ya Ndani uanzishwe ulifanya jana, na kushirikisha watu zaidi ya elfu 12 wa hali tofauti na makabilia mbalimbali.

    Akizungumza kwenye mkutano huo, Mjumbe wa kudumu wa baraza la siasa la kamati kuu ya Chama cha Kikomunisti cha China Bw. Yu Zhengsheng, ambaye pia ni mwenyekiti wa baraza la mashauriano ya kisiasa la China amesisitiza kuwa, kuanzishwa kwa mkoa huo ni mafanikio ya ubunifu wa sera mpya kuhusu sehemu za makabila madogo. Amesema Mongolia ya Ndani inapaswa kutumia vizuri zaidi sera hiyo, ili kulinda maslahi ya watu wa makabila mbalimbali, anasema,

    "Tunapaswa kushikilia mwelekeo sahihi, na kufanya vizuri zaidi kazi ya kuunganisha umoja na kujiendesha, na kuunganisha mambo ya makabila na mambo ya maeneo. Na kuiwezesha sera ya kujiendesha kwa sehemu za makabila madogo itoe mchango mkubwa zaidi kwa ajili ya kulinda umoja wa taifa, ukamilifu wa ardhi, kuhimiza usawa na mshikamano kati ya makabila tofauti, na maendeleo ya sehemu za makabila mdogo, na kuimarisha nguvu ya kushikamana kwa wachina wote."

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako