Kiyeng, bingwa wa mashindano ya jumuiya ya madola katika mbio hizo purity Kirui, na bingwa wa dunia katika mbio za mita 3000 za chipukizi Cellphine Chespol na Beatrice Chepkoech walifuzu kwa fainali itakayoandaliwa ijumaa usiku.
Kiyeng na Kirui waliongoza kwa wakati mmoja lakini ni Gesa Felicitas Krause kutoka Ujerumani ambaye alishinda nusu fainali ya kwanza. Kiyeng, aliyeshinda medali ya fedha kwenye mashindano ya Olimpiki ya Rio mwaka uliopita, alimaliza wa pili akifuatiwa na Kirui.
Hata hivyo, Chepkoech na Chepsol walishinda nusu fainali zao bila kutoa jasho na kuwezesha Kenya kuwa na nyota wanne katika fainali kuamua nani atatwaa medali siku ya Ijumaa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |