Mahakama nchini China zimeanza kufuatilia uhalifu unaohusu masuala ya fedha kwenye mtandao wa Internet ili kulinda maendeleo mazuri ya sekta hiyo.
Mwongozo uliotolewa na Mahakama Kuu ya China hii leo umesema, shinikizo ni lazima liwekwe kwenye kupambana na uchangishaji fedha haramu, ambalo ni suala muhimu katika kudhibiti hatari za kifedha. Mwongozo huo umesema katika kushughulikia kesi kama hizo, mahakama zinatakiwa kushirikiana na mamlaka husika ili kulinda maslahi ya waathirika.
Mwaka jana, zaidi ya watu elfu 16 walifikishwa mahakamani kwa makosa mbalimbali yanayohusiana na uhalifu wa kifedha.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |