Kwa ushindi huo sasa rasmi Wallace Karia atatawala nafasi ya Rais wa TFF hadi 2021 makamu wake akiwa ni Michael Richard Wambura aliyewashinda wagombea wenzake wengine watano.
Punde baada ya kutangazwa mshindi, Karia alisema mchezo wa soka unapendwa na watu wengi lakini kutokana na ubadhirifu, wadhamini wanakimbia, na sasa yeye lengo lake kubwa ni kurejesha hadhi ya soka.
Karia anachukua nafasi ya Jamali Malinzi, aliye enguliwa kwenye uchaguzi huo kutokana na tuhuma za ubadhirifu wa fedha za TFF, yeye na Katibu Mkuu wa TFF, Selestine Mwesigwa.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |