• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Usajili wa mtandao ulipungua kwa asilimia 3.6

    (GMT+08:00) 2017-08-14 19:25:24
    Usajili wa mtandao ulipungua kwa asilimia 3.6 ikilinganishwa na robo ya mwisho, ripoti ya hivi karibuni kutoka kwa mamlaka ya mawasiliano inaonyesha.

    Takwimu za robo ya tatu mwaka wa fedha 2016-2017 kuanzia Januari hadi Machi 2017, ilibainisha kuwa usajili ulishuka hadi milioni 25.7 kutoka milioni 26.6 katika robo ya mwisho.

    Hata hivyo, idadi ya watumiaji wa intaneti iliongezeka kwa asilimia 2.3 na inakadiriwa watumiaji wameongezeka hadi watu milioni 40.5 kutoka milioni 39.6.

    Kwa upande mwingine, idadi ya usajili wa mtandao ilikua kwa asilimia 3.4 ikilinganishwa na kipindi hicho cha mwaka uliopita.

    Takwimu za simu za mkononi na usajili wa intaneti zilifikia milioni 21.5 au asilimia 99 ya jumla ya usajili wa mtandao wakati wa robo ya ukaguzi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako