Ajali za barabarani zilizotokea nchini Ethiopia katika mwaka jana zilisababisha vifo vya watu 4,500, idadi ambayo ilipungua kwa asilimia 4.4 kuliko mwaka uliotangulia. Mkurugenzi mkuu wa mamlaka ya uchukuzi ya Ethiopia Bw. Kassahun Hailemariam amesema hatua zilizochukuliwa na mamlaka hiyo za kuimarisha usalama barabarani zimechangia kupungua kwa vifo vinavyotokana na ajali za barabarani.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |