• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Mauzo ya chai ya Rwanda yaongezeka

    (GMT+08:00) 2017-08-15 19:12:12
    Rwanda ilipata dola milioni $8.6 kutoka kwa mauzo ya chai kufikia mwezi Juni mwaka huu.

    Taakwimu kutoka kwa halamashauri ya kuuza bidhaa za kilimo nje ya nchi (NAEB) zinaonyesha kwamba mauzo ya mwaka jana kipindi sawa na hicho yalikuwa dola milioni 6.1.

    Ongezeko la mapato limechangiwa na kuimarika kwa bei kwenye soko la kimataifa ambayo sasa ni dola $3.38 kwa kilo ikilinganishwa na dola $2.43 za mwaka jana.

    Aidha chai iliouzwa na Rwanda mwaka huu imeongezeka.

    NAEB inasema ilenga kupata dola milioni $94.9 kwa mwaka ifikapo mwaka 2018.

    Hadi sasa serikali imegawa zaidi ya miche milioni 13 za chai ili kuongeza uzalishaji.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako