Timu ambazo zimethibitisha kushiriki kwao kwenye mashindano hayo ni ile ya mabingwa watetezi Rwanda Revenue Authority, Chuo kikuu cha Kibungo (UNIK), Kigali Volleyball Club (KVC), Chuo kikuu cha Utalii na teknologia (UTB), Gisagara, Rwanda Energy Group (REG), pamoja na timu ya wanaume na kinadada ya APR.
Timu za ugenini zitakazoshiriki mashindano hayo ya siku mbili ni kama vile Muzinga na Rukinzo kutoka Burundi, Kenya Administration Police, Prisons, Corporative Bank na Nairobi City Council.
Idadi kamili ya jumla ya timu zitakazoshiriki mashindano hayo inatarajiwa kuongezeka hadi 36 kutoka timu 22 zilizoshiriki mwaka uliopita.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |