Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Bibi Hua Chunying amesema pendekezo la China kuhusu kujenga "Ukanda Mmoja na Njia Moja" linaendana na mwelekeo wa maendeleo na maslahi ya watu wa nchi mbalimbali, na yana mustakabali mzuri.
Amesema China inapenda kushirikiana na nchi mbalimbali kujenga "Ukanda Mmoja na Njia Moja" kwa kanuni za kujadili, kujenga na kunufaika pamoja.
Habari zinasema hivi karibuni waziri wa maendeleo ya taifa wa Singapore Bw. Lawrence Wong amesema pendekezo la China kuhusu "Ukanda Mmoja na Njia Moja" litabadili maendeleo ya Asia katika kipindi kijacho, na litakuwa jukwaa kubwa zaidi la ushirikiano wa kikanda.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |