Mwanariadha huyo mwenye umri wa miaka 24, ambaye pia anahudumu kama afisa wa polisi nchini Kenya, aliwaongoza Wakenya wenzake na kumaliza nafasi ya kwanza na ya pili katika mbio za mita 1500 za wanaume na kurejesha ubabe wa Kenya katika mashindano hayo.
Manangoi kwa sasa anaongoza katika jedwali katika mbio hizo kabla ya mashindano mawili ya mwisho ya msimu huu zitakazoandaliwa katika miji ya Zurich na Brussels.
Yeye ni Mkenya pekee kati ya mabingwa wa dunia 18 walioalikwa kushiriki mashindano ya Weltklasse Diamond League jijini Zurich Agosti 20.
© China Radio International.CRI. All Rights Reserved. 16A Shijingshan Road, Beijing, China. 100040 |