• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Umoja wa Mataifa wasema idadi ya wakimbizi wa Sudan Kusini nchini Uganda yafikia milioni moja

    (GMT+08:00) 2017-08-17 16:57:00

    Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limesema, idadi ya wakimbizi wa Sudan Kusini nchini Uganda imefikia milioni moja.

    Shirika hilo limesema, zaidi ya mwaka mmoja uliopita, kiasi cha raia 1,800 wa Sudan Kusini walikuwa wakiingia nchini Uganda kila siku. Shirika hilo pia limesema, licha ya wakimbizi hao wa nchini Uganda, wakimbizi wengine milioni moja au zaidi wa Sudan Kusini wanahifadhiwa nchini Sudan, Ethiopia, Kenya, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, na Jamhuri ya Afrika ya Kati.

    Aidha, Shirika hilo limesema zaidi ya asilimia 85 ya wakimbizi wa Sudan Kusini waliokimbilia Uganda ni wanawake na watoto.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako