• Idhaa ya Kiswahili
  • Uchumi
  • Michezo
  • Facebook
  • ChinaABC
  • Sayansi
  • Afya
  • Benki ya Maendeleo ya BRICS yafungua tawi la kwanza barani Afrika

    (GMT+08:00) 2017-08-18 18:32:26

    Tawi la kwanza la Benki ya Maendeleo ya BRICS limefunguliwa hivi karibuni nchini Afrika Kusini.

    Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya China Bibi Hua Chunying ametoa pongezi kwa ufunguzi wa tawi hilo, na kusema China itatoa mchango kuzisaidia nchi za Afrika kujiendeleza.

    Msemaji huyu amesema Benki ya Maendeleo ya BRICS ni sehemu muhimu ya utaratibu wa ushirikiano kati ya Brazil, Russia, India, China na Afrika Kusini, na injini ya maendeleo ya pamoja ya nchi hizo. imeongeza nguvu mpya kwenye ushirikiano wa kusini na kusini.

    China itaandaa mkutano wa 9 wa viongozi wa nchi za BRICS mjini Xiamen tarehe 3 hadi tarehe 5 Septemba, na inatarajia kushirikiana na pande mbalimbali kuuhimiza mkutano huo kupata mafanikio mengi.

    Webradio
    Sauti
    6:00-7:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 1
    12:00-13:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 2
    20:00-22:00 (Afrika Mashariki)
    • FM 3A
    • FM 3B
    Maoni yako